User:Robert Ullmann/Mwananchi/9 January 2009

From Wiktionary, the free dictionary
Jump to navigation Jump to search

User:Robert Ullmann/Mwananchi/header

afya
Kwa hiyo basi, tunawaomaba wananchi wa Zanzibar kuendelea na juhudi za kukabiliana na ugonjwa huo, kwa kuzingatia kanuni za afya ambazo ndiyo kinga pekee muhimu kwa ugonjwa huo. [1]
amani
Mbali na kosa hilo la kutusi, upande wa Jamhuri ambao ndio mlalamikaji katika makosa yote ya jinai unaweza kuongeza na kosa la kutishia amani kwa kughadhibisha watu wengine. [2]
ana
Danny ana maumivu fulani nina wasiwasi sana na lakini mpaka kesho (leo) asubuhi nitajua lakini hana hali mbaya sanaanasema Daktari wa timu, Juma Sufian. [3]
bado
Kuhusu mvutano uliokuwapo kati yake na Mengi akijibu maswali ya waandishi Masha alisema, suala Mengi halijakwisha kwani bado wanasubiri ushahidi wake aliosema ili waweze kufuatilia tuhuma alizotoa. [4]
baina
Mazungumzo baina ya CCM na CUF yaliingia kwenye mtafaruku baada ya chama hicho cha upinzani kutangaza kuwa kimejitoa kwa kuwa wenzao wanakiuka makubaliano. [5]
bali
Katika hotuba hiyo, Green alisema, CCM na CUF havipaswi kuwekeana uadui bali vinapaswa kujadiliana na kuangalia mfumo ambao utamaliza tatizo la kisiasa Zanzibar hasa ikizingatiwa kuwa vyama vyote vina wafuasi wanaolingana. [6]
basi
Mimi namshukuru mume, watoto wangu na familia yangu kwa ujumla maana uchaguzi ulikuwa ni mgumu haijapata kutokea na kusema kweli uchaguzi ulikuwa na rafu nyingi sana, hata hivyo kama mshindi kapatikana basi tutamuunga mkono kwa dhati," alisema mama Kahama. [7]
bei
PAMOJA na jitihada za serikali kuwataka wafanyabiashara wa mafuta nchini, kushusha bei ya nishati hiyo, wauzaji wa jijini Dar es Salaam, wameendelea kukaidi amri hiyo kwa kuendelea kuuza mafuta kwa bei ya juu. [8]
chanjo
Chanjo ya kipindupindu isiwalemaze wananchi JUZI Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), ilitangaza kuwa Januari17, mwaka huu itaanza kuifanyia majaribio chanjo mpya ya ugonjwa wa kipindupindu katika visiwa vya Unguja na Pemba, ikiwa ni juhudi zake za kutokomeza ugonjwa huo visiwani humo. [9]
dawa
Alisema, mbali na hilo jeshi la polisi kwa ushirikiano na vyombo vingine vya dola, limekamata watuhumiwa 22,092 na kilo 133 za dawa za kulevya za viwandani na jumla ya watuhumiwa 19,409 walikamatwa na kilo 512,898 za bangi na ekari 653 za mashamba ya bangi zimeteketezwa. [10]
dhidi
Kuna majibizano makali kutoka kwa baadhi ya wafuasi kwenda kila upande wa siasa dhidi ya wapinzani wao. [11]
dizeli
Kwa upande wa mafuta ya dizeli bei iliyopo kwenye mabango ya vituo vingi vya mafuta inaonyesha kuwa ni Sh. [12]
eneo
Walitengeneza funguo bandia na baada ya mmiliki wa gari hilo kuliweka katika eneo la kupaki huko Nansana, watu hao walirejea na kuwadanganya walinzi kuwa mmiliki amewatuma kuichukua gari hiyo," alinena Nabakooba. [13]
es
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Masha alisema mamlaka ya vitambulisho hivyo imeshaundwa na matarajio ni kuwa, vitambulisho vitaanza kutolewa mwaka huu. [14]
haja
Hivyo, kuna haja kuwa na utaratibu au kampeni maalumu ya kuwasaka watu wa aina hiyo kuanzia kwenye maduka ya dawa hadi kwa waganga wa jadi na wanaopatikana navyo wachukuliwe hatua za kisheria. [15]
hali
Aliesma kuwa hali ikiendeea namna hiyo UWT itakuwa haina mwelekeo kabisa na haionyeshi mfano bora kwa jumuiya zingine kutokana na kutawaliwa na matusi wakati wa kampeni. [16]
hao
Alisema changamoto kubwa ni uhalifu wa mauaji ya albino ambapo alisema kuwa, serikali itapambana na kufanya kila iwezalo kuhakikisha wauaji hao wanadibitiwa. [17]
haraka
Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasilianio Ikulu baada ya mazungumzo ya Rais Kikwete na mabalozi hao, ilisema, rais amezitaka Palestina na Israel kutafuta haraka njia za kukomesha mapigano yanayoendelea huko Gaza. [18]
hata
Kwa upande wake, Janet Kahama aliuponda uchaguzi huo na kusema kuwa ulikuwa na kasoro nyingi yakiwemo matusi amabayo hayaelezeki na kwamba, hata mumewe alitukanwa kwa ajili yake. [19]
hatua
Katika hatua nyingine, Green alifafanua kuwa kitendo cha Marekani kusaidia wananchi wa Tanzania ni sehemu ya kupunguza uhasama nchini mwake. [20]
haya
Rais (George) Bush ameyafanya haya, kama alivyofanya aliyemtangua Rais Clinton. [21]
hayo
Kahama ambae alifika ukimbini muda mfupi kabla ya matokeo hayo alionyesha kutokuridhika kabisa na jinsi mchakato uchaguzi ulivyoendeshwa. [22]
hii
Huu ni mwaka wa 2009 ambayo jumla ni 11, awamu hii ya nne chini ya uongoz i wa CCM ni miaka 47 ambayo 4+7 = 11. Kwa hiyo herufi ya kumi ni J na ya 11 K yaani JK ndie mshindi" alitabiri sheikh Yahya. [23]
hili
Baadhi ya wafanyakazi wa shirika hilo waliozungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti jana, walikiri kuwa miongoni mwao tayari wameenda benki na kuthibitisha kuwa mishahara imeingia kwenye 'akaunti' zao. [24]
hivi
Alisema, hadi hivi sasa zaidi ya watuhumiwa 100 wa mauaji ya albino wamekamatwa na mashauri yao yako katika hatua mbalimbali za kushughulikiwa kisheria. [25]
hizo
Aliwatoa hofu Watanzania akisema kuwa hata baada ya Rais Bush kumaliza muda wake, Rais Obama naye utaendelea juhudi hizo za kuisaidia Tanzania. [26]
huku
Muda wa kutangazo matoke, Ukumbi wa Kilimani mjini Dodoma, ulipofanyika mkutano huo ulitulia kimya huku wajumbe wakisubira jina mshindi. [27]
huo
Kwa ujumla, wimbo huo uliambatana na shamrashamra na wanawake waliokuwa kwenye Mkutano Mkuu wa Saba wa UWT, licha ya matatokoe kutokuwa tayari, uliaashiria wazi kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Sophia Simba alikuwa ameshinda na hatimaye akwa hivyo. [28]
husika
Anasema tayari kazi ya kubaini maeneo zitakapopita barabara husika imekwishafanyika hivyo yeyote atakayeanza ujenzi mpya katika maeneo hayo yuko katika hatari ya kuingia hasara ya kutolipwa fidia yoyote na majengo yake kuondolewa. [29]
huu
Alidokeza kuwa viongozi wana wajibu wa kuwaelekeza wafuasi wao juu ya ukweli huu na kuwasahihisha wale wanaoweka maslahi ya chama mbele badala ya maslahi ya wananchi. [30]
ila
Alisema historia ya Zanzibar haitofautiani na ile ya Marekani, ila walichokifanya wao katika kuondoa tofauti zao ni kuwa na mfumo wa kugawana madaraka na ndio hadi sasa umeweza kujenga umoja wa taifa hilo lenye nguvu duniani. [31]
ina
Akizungumza na balozi wa Israel, Kikwete alisema," ni kweli Israel ina haki ya kujilinda dhidi ya mashambulizi ya Hamas, lakini bado taifa hilo limetumia nguvu nyingi katika kulipiza kisasi. [32]
jadi
Taarifa zilizoenea sehemu mbalimbali nchini; na hata kukamatwa na kushtakiwa mahakamani kwa mganga mmoja wa jadi kwa tuhuma za kukutwa na vifaa mbalimbali vya hospitalini na madawa kadhaa, zinadhihirisha kuwa vifaa hivyo sasa vinatumiwa na watu wasio na sifa kutumia vifaa hivyo kutibu wagonjwa. [33]
jiji
Foleni katika barabara mbalimbali za jiji hili kubwa zaidi nchini umekuwa ukisababisha wakazi wake wengi kupoteza muda mwingi njiani na hivyo kuharibu mipango mingi ya uzalishaji mali na hata huduma za kijamii. [34]
jioni
Waganda katika mchezo wa leo wa kumalizia kundi B,utakaochezwa kwenye uwanja wa Nakivubo mjini Kampala Uganda majira ya saa 10 jioni. [35]
juzi
Uchaguzi huo ulisimamiwa Seif Khatib akisaidiwa na Dk Abdalah Kigoda na Yusuf Omary Mzee ambao walikuwepo katika mkutano huo tangu juzi hadi jana ulipofungwa. [36]
kambi
Nataka wazoee mazingira ya kambi na maisha ya timu ya Taifa ili wakati tukitoka Ivory Coast nitakapobadili kikosi wasiwe wageni. [37]
kanuni
Akizungumza katika mkutano huo wa hadhara uliofanyika baada ya Kamati ya Maendeleo ya Kata, Mstaahiki Meya wa Manispaa ya Temeke, Jerome Bwanausi, amesema kitendo hicho ni ukiukwaji wa kanuni, taratibu na sheria za manispaa. [38]
kasi
Uganda ambayo katika mechi dhidi ya Somalia ilionekana kubadilika, mashabiki wake wameshtushwa na kipigo ilichotoa Stars wanaogopa zaidi safu ya ushambuliaji iliyojaa wachezaji wenye kasi. [39]
kati
Akitangaza matokea ya uchaguzi huo, mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Seif Khatibu alimtangaza Simba kuwa alikuwa amepata kura 470 sawa na asilimia 54.5 ya kura zote zilizopigwa na kuwaacha washindani wake, Janet Kahama aliyepata kura 383 sawa na asilimia 48.4 na Joyce Masunga aliyeambulia kura 10 sawa na asilimia 1.1 kati ya kura halali 862 zilizopigwa. [40]
kazi
Aklitoa shukurani baada ya matokeo ya uchaguzi huo kutangazwa, Joyce Masungu aliyewania nafasi ya mwenyekiti, aliaahidi kushirikiana na mama Simba akisema kuwa yuko tayari kufanya kazi za UWT na CCM wakati wowote atakapotumwa na mwenyekiti wake. [41]
kesho
Mpinzani wa leo anaweza kuwa rafiki wa kesho. [42]
kiafya
Hata hivyo, Mkurugenzi wa Afya na Ustawi wa Jamii wa SMZ, Juma Rajab amesema kutokana na tahadhari ya kiafya, wanawake wajawazito hawatapewa dawa hiyo kwa kuwa, bado hakuna taarifa za utafiti wa madhara yake kwa akina mama wajawazito. [43]
kiasi
Nashawishika kusema kwamba kiasi kikubwa cha maumivu ya kisiasa ya Zanzibar yametokana CCM kukitenga CUF kisiasa," alisema Green. [44]
kikao
Mara nyingi nimekuwa nikipata bahati ya kuwepo kwenye kikao cha usuluhishi wa migogoro mingi ya wanandoa. [45]
kila
Hakuna kiongozi atakayeweza kuendesha kila kitu anavyotaka yeye milele. [46]
kuanza
Pamoja na hali hiyo, baadhi ya wafanyabiashara wameonekana kuanza kushusha bei hiyo. [47]
kujifunza
Kwa mfano, katika kujifunza lugha na elimu inayohusiana na viungo vya kijinsia. [48]
kulinda
Kuthibiti lina maana ya kuwa ya kweli, kuwa ya kuaminika ambapo kudhibiti ina maana ya kulinda, kutia mkononi, kutunza. [49]
kuna
Ukweli ni kwamba kuna majambazi wengi wa magari ambao wana uhusiano naye wa karibu. [50]
kutoa
Ofisi ya mradi wa vitambulisho imepatikana, mratibu wa mradi ameteuliwa na mchakato wa kumpata mkandarasi wa kutoa vitambulisho unaendelea," alisema Masha. [51]
kutoka
Kwa upande wa wajumbe wa Baraza Kuu kutoka Tanzania bara walioshinda ni Bety Machangu, Magret Mkanga, Sifa Swai, kutoka Zanzibar ni Ratifa Nasoro, Subira Ally, Mtumwa Yusufu, Lilian Limo na Catherin Nao. [52]
kuwepo
Rais Kikwete pia alisisitiza msimamo wa Tanzania wa kutaka kuwepo kwa mataifa ya Israel na Palestina katika eneo hilo la Mashariki ya Kati. [53]
la
Simba aliuomba mkutano mkuu wa saba kumkubalia Anna Abdalah kuwa mjumbe wa kudumu wa Baraza Kuu la UWT na kukubaliwa na wajumbe wote. [54]
lazima
Ni lazima kueleza hapa kuwa Serikali inalaani vikali mauaji haya na itafanya kila liwezekanalo kuhakikisha kuwa wauaji wanadhibitiwa," alisema Masha. [55]
lengo
SHIRIKISHO la soka Tanzania (TFF) limeijibu klabu ya Mtibwa Sugar kuwa haijawahi, haina na haitakuwa na lengo la kutoa tamko kwa ajili ya kumdhalilisha mtu, kundi la watu au wanachama wake kama ilivyo kwa timu hiyo. [56]
ligi
Kocha mpya wa timu hiyo ya mtaa wa Msimbazi Mzambia, Patrick Phiri jana alitia saini mkataba wa miaka miwili wa kuifundisha timu hiyo huku akiwahakikishia wapenzi na wanachama sasa Simba itarudi kwenye nafasi ya kwanza katika msimamo wa ligi. [57]
lina
Kundi hilo lina timu za Senegal, Zambia na wenyeji Ivory Coast. [58]
lita
Ufuatiliaji wa bei ya mafuta jijini hapa uliofanywa na Mwananchi, unaonyesha kuwa vituo vingi vya mauzo vinauza mafuta ya petroli kwa bei kati ya Sh1,600 hadi Sh1,400 kwa lita kinyume na bei ya Sh 1,166 iliyopangwa na serikali. [59]
lugha
Ninachunguza matumizi ya maneno na miundo ya sentensi kwa lengo la kuwatanabaisha waandishi na wasomaji kuwa ufasaha wa lugha ni jambo la kuzingatiwa ili tuweze kuulinda utamaduni wetu tulioachiwa na wazee wetu pamoja na kuuendeleza kwa ajili ya vizazi vijavyo. [60]
madai
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza, Jamal Rwambow, alisema uchunguzi huo unalenga katika kupata ushaidi juu ya madai kuwa marehemu alikufa kwa kipigo cha mama yake wa kambo. [61]
maeneo
Shirika la ndege ni moja ya vivutio vikubwa vya utalii, kwa sababu kuwepo kwake kunaweza kuwahamisha watalii kuja nchini kwa kuwa na uhakika wa usafiri katika maeneo mbalimbali, ndani ya nchi na hata kutoka nje. [62]
mila
Katika mchakato mzima wa uundaji wa sheria mbalimbali, dhana ya mazingira hugusa maeneo mengi zaidi ikiwa ni pamoja na hali ya kisiasa, kiuchumi na wakati mwingine hata kijiografia, lakini zaidi ni muhimu kuhusisha na kuzingatia mila na desturi za jamii husika ambayo kwa ajili yake sheria husika inakusudiwa kutungwa au kuundwa. [63]
mingi
Kaimu mkuu wa RRU, Asuman Mugenyi, alisema Mchungaji Kizito amekuwa akituhumiwa kwa wizi wa magari nchini Uganda kwa miaka mingi na kuyauza DRC, na kwamba amekiri kwa Polisi kuwa amekuwa akifanyakazi hiyo kwa miaka 15 sasa. [64]
mkuu
Kwa upande wa wawakilishi wa jumuiya za CCM walioshinda na Martha Mlata ambae atakuwa ni mwakilishi kwa Jumuiya ya wazazi na upande wa vijana alichaguliwa Shy-Rose Bhanji ambaye alimshinda mbali mkuu wa wilaya ya Mpwapwa, Halima Dendego. [65]
mmoja
MABALOZI wa nchi za Israel na Palestina jana walipishana Ikulu jijini Dar es Salaam, wakati kila mmoja akimfuata Rais Jakaya Kikwete, kwa mazungumzo na utambulisho. [66]
moja
Haipaswi kundi moja la kisiasa lijisikie limetengwa na Serikali. [67]
mpaka
Mathalani, wiki iliyopita vituo vya BP, vilikuwa vinauza petroli kwa Sh1,470 na jana bei hiyo ilikuwa Sh1,402 kwa lita na dizeli kushuka kutoka Sh1,450 mpaka Sh1,233 kwa lita. [68]
mpya
Akihutubia mkuwatano huyo baada ya kutangazwa mshindi, Mwenyekiti mpya alisema kuwa atashirikiana na wajumbe wote pamoja na kuandaa semina kwa wote waliochaguliwa kushika nafasi mbali mbali katika umoja huo. [69]
mtu
Nimewaambia wachezaji kila mtu asimame na mtu kuanzia mwanzo mpaka mwisho, wasitoe nafasi wachezee mpira, watulie halafu wanapanga mashambulizi. [70]
muhimu
Katka vituo hivyo bei ya dizeli juma lililopita ilikuwa Sh1,450 lakini jana bei hiyo ilishuka mpaka kufikia Sh 1,233 kwa lita, hali inayowapa wananchi matumaini ya kushuka kwa bei ya nishati hiyo muhimu kwa ukuaji wa uchumi. [71]
mwa
Kwa sababu hiyo, Green alivishawishi CCM na CUF, kuacha uadui na badala yake kurejea kwenye meza ya mazungumzo ya muafaka wa kisiasa hasa ikizingatiwa kuwa chokochoko za kisiasa zimetawala miongoni mwa wafuasi wao. [72]
nane
Tunawajua katika namba saba na nane wako vizuri sana, kuna wachezaji kama Bengo Stephen, Tonny Mawejje, Massa Geofrey ni hatari sana na hatupaswi kuwapa nafasi kabisa. [73]
naye
Rais Mteule Obama naye amefanya hivyo hivyo," alibainisha Green. [74]
ndani
Aidha, amesema kuwa serikali hiyo ya muungano wa vyama itaongozwa na rais aliyepo madarakani Jakaya Kikwete kutokana upinzani aliouonyesha ndani ya Chama na serikali yake. [75]
neno
Ukweli ni kwamba mwandishi alikuwa na lengo la kutumia neno kudhibiti. [76]
nje
Hakuna chama kinachoshinda madaraka kwa asilimia 100. Hakuna chama kilicho nje kabisa ya mfumo wa madaraka. [77]
nne
Akizungumzia ripoti ya mafanikio ya miaka mitatu ya serikali ya awamu ya nne kwa wizara yake Masha alisema kuwa, wizara hiyo inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na msongamano wa wafungwa magerezani, wahamiaji haramu na kuongezeka kwa uhalifu. [78]
nusu
Katika mchezo wa kuwania kufuzu nusu fainali ya kombe la Chalenji, ambao asilimia hamsini ya Stars wana malaria, Uganda haina cha kupoteza lakini Stars inahitaji ushindi huku ikisikilizia matokeo ya mechi ya nyingine. [79]
pekee
Nafasi ya Makamu wa Mwenyekiti ilikwendaka kwa Asha Bakari Makame ambaye alikuwa mgombea pekee, aliyepata kura 736 sawa na asilimia 60.3 na kura 70 zilimkataa. [80]
rais
Miongoni mwa miradi hiyo ambayo ilipewa msukumo mkubwa na rais anayemaliza muda wake, George Bush ni mpango wa kupambana na Ukimwi, Malaria na Millennium Challenge ambao utaboresha miradi mbalimbali ukiwepo wa kuboresha na kuunganisha umeme Unguja na Pemba. [81]
saa
Mtoto huyo alifariki dunia Novemba 19 mwaka jana na kuzikwa siku Iliyofuatia katika makaburi ya Nyasaka na kaburika lake lilifukuliwa saa 5:34 ya asubuhi ya jana chini ya usimamizi wa Inspekta wa Polisi Inongu Kinasa. [82]
sita
Uganda ina pointi saba huku Stars ikiwa na sita zikishikilia nafasi mbili za juu kwenye kundi A ambalo hatma yake itajulikana leo. [83]
sugu
Kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa na SMZ, chanjo hiyo ni ya kwanza kutolewa nchini Tanzania na kwamba, wameshaandaa maeneo maalumu ya kufanyia majaribio hayo, ambayo ni yale yenye matatizo sugu ya ugonjwa huo visiwani humo na watu 5,000 wakiwemo watu wazima na watoto wanaotarajiwa kuchanjwa. [84]
uamuzi
Neno maamuzi lilitakiwa liwe uamuzi. [85]
vazi
Mimi siwezi kusema vazi fulani halifai kuvaa ila vazi linafaa kwa mahali husika; Katika sentensi hii neno lisilofaa hapa ni kuvaa. [86]
vya
Hali ya hewa kisiasa hapa visiwani itaimarika iwapo viongozi wa vyama vikuu vya kisiasa watatangaza hadharani kwamba wanawaheshimu wapinzani wao kama ni Wazanzibari na Watazania walio wazalendo. [87]
wa
Hivi ndivyo walivyokuwa wakiimba baadhi ya akina mama katika baadhi ya mitaa ya mji wa Dodoma jana kabla ya matokeo uchaguzi wa Mwenyejkiti wa Jumumia ya wananwake wa Chama cha Mapinduzi (UWT) taifa kutangazwa. [88]
wala
WAZIRI wa Mambo ya Ndani Lawrence Masha, ameendeleza ngonjera katika suala la vitambulisho vya uraia kwa kusema vitaanza kutolewa mwaka huu bila kutaja siku, mwezi wala tarehe ya kutolewa kwa vitambulisho hivyo. [89]
wawili
Nimepokea malalamiko kutoka kwa wazazi wawili ambao watoto wao walikuwa wakisoma katika shule za msingi Mtoni Kijichi na Bwawani. [90]
wengi
Watu wengi walitafsiri vibaya nilipotoa siku saba Mengi awasilishe ushahidi wake, tulikuwa tunataka tupate ushahidi huo ili tuweze kufuatilia tuhuma alizotoa, siku saba zimepita na hakuleta ushahidi lakini bado suala halijakwisha tunasubiri awasilishe ushahidi ili tufuatilie," alisema Masha. [91]
wetu
Wakati fulani huko nyuma baadhi ya watoa habari wetu waliwahi kukamatwa kwenye eneo hilo na waliachiwa baada ya Uganda kuingilia kati. [92]
wizi
MCHUNGAJI Mkuu wa Kanisa la Kawuku Miracle Center wilayani Wakiso,Uganda, Godfrey Kizito, amekiri kujihusisha na wizi wa magari na kuyauza katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. [93]
yao
Chiligati aliwatoa wasiwasi wananchi wa kudhulumiwa haki yao ya kupata vitambulisho hivyo, kusumbuliwa au kunyanyaswa na kusema atahakikisha kila Mtanzania wa kweli anakuwa nacho na asiyestahili hakipati. [94]
yetu
Maoni yetu ni kwamba lazima mtafute njia za haraka kukomesha jambo hilo vinginevyo msimamo wa dunia utawageuka. [95]
yote
Hivi karibuni, Waziri wa Miundombinu, Dk Shukuru Kawambwa alisema kuwa serikali imefuta madeni yote ya ATCL, lakini taarifa zilizolifikia gazeti hili zilieleza kuwa tamko hilo ni la maneno tu kwa sababu halijafanyiwa utekelezaji. [96]
za
Hali hiyo pamoja na pilipilika za maandali sherehe ya kumpongeza zilizoashiria kuwa baada ya matokea kutangazwa kungekuwa na haflakubwa ya kumpongeza waziri huyo kwa ushindi wake. [97]
zaidi
Alisema macho ya wizara hiyo yangeelekezwa zaidi katika utambulisho huo ili kuhakikisha unafanywa kwa umakini. [98]
zake
HATIMAYE wafanyakazi wapatao 300 wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL), wameanza kulipwa malimbikizo ya mishahara yao ya Novemba na Desemba, mwaka jana, huku hatima ya kuanza safari zake ikiwa bado haijulikani. [99]
zao
Kabla ya hapo, Makamu mwenyekiti wa CCM Tanzania bara, Pius Msekwa alimtaka Simba kutumia uzoefu alionao kutoka Ikulu kuwasaidia wanawake wenzake, kuhakikisha kuwa wanapata haki zao ya kimsingi. [100]